Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AUTISM SPECTRUM DISORDER-USONJI

HIZI HAPA NI DALILI ZA USONJI


1.Tatizo la kuchangamana na jamii

👉Anakuwa na changamoto wakati wa kutengeneza marafiki

 👉Anakuwa na changamoto kwenye kushiriki furaha au mafanikio yake.

 👉Mtoto anakuwa anajitenga na wengine na kupendelea kukaa pekee yake

·        👉kukwepesha macho wakati anapokuwa anaangaliana na wengine au akiangaliwa.


 2.Tatizo katika mawasiliano 

👉Kushindwa kuongea ingali umri wa kuongea umefika 

👉Changamoto kwenye kuanzisha na kuhimili au kuendeleza mazungumzo

👉Kurudia maneno unayo mwambia anakuwa hana uwezo wa kujibu zaidi ya kurudia unachomwambia 

3. Tabia za kijirudiarudia 

·   👉 Hii huhusisha mtoto kuwa na tabia za kujiumiza kama vile kujipigiza kwenye vitu,kubamiza vitu kama mlango,kupanda sehemu za juu akitaka kujirusha.

·   👉 kupenda kutembeatembea,

·   👉kufunika masikio kwenye sauti kubwa na wengine kupendelea sauti kubwa

·   👉kufumba macho kwenye mwanga mkali

·   👉kukataa mabadiliko ya vitu mfano chakula ,sehemu ya kulala, eneo jipya tofauti na alilolizoea

·   👉kucheka bila sababu hata kama wengine hawaoni sababu za kucheka


Ukiona dalili hizi anazo mwanao, mtoto wa rafiki,ndugu yako basi tupigie kwa namba zifuatazo;


Ndamo Rehabilitation Solutions Center 

Mwanza Dispensary,Mecco Kusini-Majanini

Phone:0748199113/0629199113

Email: daniellysamweli88@gmail.com



Maoni